2015 WACHEZAJI BORA AFRIKA NI SAMATTA NA AUBAMEYANG

Pierre-Emerick Aubameyang mshambuliaji wa timu ya taifa ya soka ya Gabon na klabu ya Borrussia Dortmund ya Ujerumani, ndio mchezaji bora wa mwaka 2015.
Aubameyang mwenye umri wa miaka 26 alipewa tuzo hiyo jijini Abuja jana usiku baada ya kupata alama 143 mbele ya mshambuliaji wa Manchester City na Cote Dvoire Yaya Toure aliyepata alama 136.
Mbwana Samatta kushoto na Pierre-Emerick Aubameyang kulia
Andre Ayew, kutoka Ghana na anayechezea klabu ya Swansea nchini Uingereza, alikuwa wa tatu kwa alama 112.

Aubameyang anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka Gabon kuwahi kushinda taji hili baada ya kupigiwa kura na makocha pamoja na wakurugenzi wa kiufudi kutoka barani Afrika.

Mshambuliaji huyo wa Borrussia Dortmund anaongoza kwa ufungaji wa mabao katika ligi ya Bundesliga msimu huu ,na kati ya mechi 17 alizocheza amefunga mabao 18.

Kwa upande wa wachezaji wanaocheza soka katika vlabu vya bara Afrika, Mtanzania Mbwana Samatta aliyekuwa anaichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ameshinda tuzo ya mchezaji bora na anakuwa Mtanzania wa kwanza lakini pia kutoka Afrika Mashariki kunyakua taji hili.

Share on Google Plus

About Habari Duniani

WELCOME TO MICHEZOTU (SPORTS ONLY) WHICH IS PART OF HABARI DUNIANI MEDIA GROUP. WE ALWAYS BRING TO YOU ANALYTICAL NEWS IN YOUR FINGER TIPS. TO ADVERTISE WITH US, EMAIL US VIA habariduniani@gmail.com
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment